Ili kuonyesha mshikamano wa kitaifa kwa familia ya marehemu, viongozi mbalimbali, wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, walifika nyumbani kwa familia Bweleo, Mkoa wa Mjini Magharibi, kutoa pole na faraja.

26 Septemba 2025 - 12:34

Rais Dr. Samia Suluhu Hassan na Viongozi Wengine wa Kitaifa Watoa Pole kwa Familia ya Marehemu Abbas Mwinyi - Zanzibar + Picha

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt as -ABNA- Zanzibar, (jana) 25 Septemba 2025 - Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amepokea mkono wa pole kufuatia kifo cha kaka yake, Abbas Ali Mwinyi, kilichotokea jana.

Rais Dr. Samia Suluhu Hassan na Viongozi Wengine wa Kitaifa Watoa Pole kwa Familia ya Marehemu Abbas Mwinyi - Zanzibar + Picha

Ili kuonyesha mshikamano wa kitaifa kwa familia ya marehemu, viongozi mbalimbali, wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, walifika nyumbani kwa familia Bweleo, Mkoa wa Mjini Magharibi, kutoa pole na faraja.

Miongoni mwa viongozi walioungana na Rais Samia ni:

Rais Dr. Samia Suluhu Hassan na Viongozi Wengine wa Kitaifa Watoa Pole kwa Familia ya Marehemu Abbas Mwinyi - Zanzibar + Picha

1_ Naibu Waziri Mkuu, Mhe. Dotto Mashaka Biteko

2_Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mwansasu

3_Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla

4_Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Zuberi Ali Maulid

5_Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Taifa, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro

6_Pamoja na viongozi wengine wa ngazi mbalimbali.

Rais Dr. Samia Suluhu Hassan na Viongozi Wengine wa Kitaifa Watoa Pole kwa Familia ya Marehemu Abbas Mwinyi - Zanzibar + Picha

Tarifa ya mazishi:
Marehemu Abbas Ali Mwinyi atasaliwa Masjid Jamia Zinjibar, Mazizini baada ya Sala ya Ijumaa, na kuzikwa Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja, leo tarehe 26 Septemba 2025.

Your Comment

You are replying to: .
captcha